
Nahodha na kiungo mshambuliaji wa Aston Villa, Jack Grealish.
Smith amesema “Mimi na Jack tuliamini atarejea hivi karibuni lakini amepata maumivu ya nyama za paja ambayo yatamfanya azidi kuwa nje ya wiki kwa wiki mbili”.
“Alikuwa vizuri sana mazoezini, lakini hakuweza kuvumilia na kuendelea. Ni majeraha ambayo yanamhitaji apate nafasi ili arejee”.
Taarifa hiyo itawapa simanzi mashabiki wa Aston Villa kwani nahodha huyo amefunga mabao muhimu 6 na kutengeneza mengine 12 na kuisaidia Villa kushika nafasi ya 9 wakiwa na alama 44 baada ya michezo 29.